Baadhi ya watumishi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakiwa katika picha ya pamoja katika Maadhimisho ya Siku ya Wanyakazi Duniani ( Mei mosi) iliyofanyika Kitaifa katika Viwanja vya Jamhuri Mkoani Dodoma.
Baadhi ya Watumishi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakiwa wamebeba bango lenye Ujumbe wa Maadili katika Kilele cha Siku ya Wafanyakazi Duniani ( Mei Mos) i ilizofanyika kitaifa katika Viwanja vya Jamhuri Mkoani Dodoma.
Katibu – Idara ya Ukuzaji Maadili, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Waziri Kipacha akichangia katika Kikao cha Utekelezaji wa Majukumu ya Baraza la Maadili mbele ya Mwenyekiti wa Baraza hilo Mhe. Jaji (Mst.) Ibrahim Mipawa (mbele kulia) na Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi (mbele kushoto) kilichofanyika katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Makao Makuu Jijini Dodoma tarehe 27 Aprili, 2022. Kulia kwa Bw. Kipacha ni Mjumbe wa Baraza la Maadili Bibi Suzan Mlawi.
Wakili wa Serikali Mwandamizi - Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Hassan Mayunga (kushoto) akitoa mada katika Kikao cha Utekelezaji wa Majukumu ya Baraza la Maadili kwa Wajumbe wa Baraza hilo linaloongozwa na Mhe Jaji (Mst.) Ibrahim Mipawa pamoja na Watendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kilichofanyika katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Makao Makuu Jijini Dodoma tarehe 27 Aprili, 2022.
Mjumbe wa Baraza la Maadili Bw. Peter Ilomo (kulia) akichangia katika Kikao cha Utekelezaji wa Majukumu ya Baraza la Maadili mbele ya Mwenyekiti wa Baraza hilo Mhe. Jaji (Mst.) Ibrahim Mipawa na Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi (hawapo pichani) kilichofanyika katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Makao Makuu Jijini Dodoma tarehe 27 Aprili, 2022. Kushoto ni Katibu - Idara ya Usimamizi wa Maadili Bw. John Kaole.
Mwenyekiti wa Baraza la Maadili Mhe. Jaji (Mst.) Ibrahim Mipawa (kulia) akiwa na mwenyeji wake Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi (kushoto) wakifuatilia mada kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma iliyokuwa ikitolewa na Wakili wa Serikali Mwandamizi Bw. Hassan Mayunga hayupo pichani wakati wa Kikao cha Utekelezaji wa Majukumu ya Baraza la Maadili kilichofanyika katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Makao Makuu Jijini Dodoma tarehe 27 Aprili, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Bi. Suzan Mlawi kuwa Mjumbe wa Baraza la Maadili katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Chamwino Jijini Dodoma tarehe 2 Aprili, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Bw. Peter Ilomo kuwa Mjumbe wa Baraza la Maadili katika hafla fupi iliyofanyika tarehe 2 Aprili, 2022 Ikulu Chamwino Jijini Dodoma.
Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi akiongoza kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kwa Mawaziri, Wajumbe wa Baraza la Maadili na Kabidhi Wasii Mkuu wa Serikali mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) Ikulu Chamwino jijini Dodoma tarehe 2 Aprili, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Jaji (Mst) Mhe. Ibrahim Mipawa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Maadili katika hafla fupi iliyofanyika tarehe 2 Aprili, 2022 Ikulu Chamwino Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Jenista Mhagama (Mb.) akitoa maelekezo kwa Mkarandarasi ambaye ni Wakala wa Ujenzi Tanzania (TBA) anayejenga Jengo la Ofisi za Sekretarieti ya Maadili Makao Makuu na Kanda ya Kati Dodoma wakati wa ziara yake ya kutembelea Mradi huo tarehe 31 Machi, 2022.